Kwa mara ya kwanza, mamlaka ya Kenya inazindua sensa ya wanyama pori siku ya Ijumaa.
Zoezi hilo litazinduliwa rasmi mashariki mwa Kenya katika hifadhi ya taifa ya milima ya Shimba.
Mamlaka ya wanyama pori (KWS) imesema sensa ya wanyama wa porini kitaifa imelenga kupata jumla ya idadi ya wanyama pori na eneo walipo.
"Zoezi hili litabainisha idadi ya wanyama pori waliopo na kutambua vitisho vilivyowakabili katika hifadhi," huduma ya wanyama pori imeeleza.
KWS na watafiti wa wanyama pori na taasisi ya mafunzo - taasisi huru ambayo inafanya utafiti wa hifadhi za wanyama pori na wanaowasimamia.
Kenya ina hifadhi za wanyama pori katika maeneo mbalimbali ya nchi.

No comments:
Post a Comment