Rais wa Marekani Joe Biden ametoa wito wa kufanyika uchunguzi wa kina ili kutambua chanzo cha maambukizi ya virusi vya corona.
Katika taafira yake aliyoitoa jana, Biden amesema wengi kwenye mashirika ya ujasusi ya Marekani wanaamini kuna uwezekano wa aina mbili, Kwamba binadamu aliambukizwa virusi hivyo na mnyama aliyeathirika navyo, au vilisambaa baada ya kutokea ajali kwenye maabara.
Biden amesema hakuna ushahidi wa kutosha wa kuupa uzito uwezekano mmoja kuliko mwingine.
Aidha rais huyo amesema maabara za kitaifa za Marekani zinapaswa kusaidia katika uchunguzi na ameitolea wito China kushirikiana wachunguzi wa kimataifa. Anatarajia matokeo ndani ya siku 90.

No comments:
Post a Comment