Mbwa waliopewa mafunzo maalum wana uwezo wa kugundua watu walioambukizwa virusi vya corona (Covid-19) chini ya sekunde 1 kwa kuvuta harufu tofauti wanayoitoa.
Kulingana na ripoti ya Guardian, katika utafiti uliofanywa nchini Uingereza, ilielezwa kuwa watu waliopatikana na Covid-19 hutoa harufu tofauti ambayo mbwa waliofunzwa wanaweza kugundua.
Hivyo basi, ilibainika kuwa mbwa 6 waliojumuishwa katika utafiti waligundua ugonjwa huo kwa ufanisi wa hadi asilimia 94.3 kutoka kwa nguo za watu wagonjwa wa Covid-19.
Ilielezwa kuwa mbwa ambao waligundua watu 94 kati ya kila watu 100 walioambukizwa kwa usahihi, walizidi vipimo vya PCR kwa ufanisi na kasi kwa kutoa matokeo ya ugonjwa huo chini ya sekunde 1.
Ilibainika kuwa mbwa waliofunzwa wanaweza kutambua haraka abiria wanaoshuka kutoka kwenye meli au ndege na kwamba watu hawa wanaweza kutengwa wakati wakisubiri uthibitisho wa matokeo ya vipimo vya PCR.
Baadhi ya nchi ikiwa ni pamoja na Finland, Falme za Kiarabu, Ujerumani na India, zilianza kufaidika na mbwa waliopewa mafunzo maalum katika kugundua wagonjwa wa Covid-19.

No comments:
Post a Comment