Malkia wa Zulu, Mantfombi Dlamini Zulu, anatarajiwa kuzikwa katika sherehe ya faragha mkoani KwaZulu-Natal nchini Afrika Kusini.
Alifariki ghafla mjini Johannesburg wiki iliyopita, karibu mwezi mmoja baada ya kifo cha mume wake, Mfalme Goodwill Zwelithini.
Familia haijatangaza hadharani chanzo cha kifo chake.
Licha ya sherehe kubwa, wasichana wa Kizulu waliofuata na mwili wa Malkia Mantfombi kurudi ikulu yake Jumatano jioni.
Uamuzi wa atakayeongoza ufalme wa Zulu unatarajiwa kutolewa baada ya mazishi.

No comments:
Post a Comment