Jumuiya ya Ulaya (EU) ilikosoa vikali uchapishaji wa orodha ya "nchi zenye uhasama" na Urusi.
Kulingana na ripoti ya Sputnik, Josep Borrell, Mwakilishi Mkuu wa EU wa Maswala ya Kigeni na Sera ya Usalama, alitaka kutafakariwa tena kwa uamuzi huu ili kuzuia kuzorota zaidi kwa uhusiano "uliodhoofishwa."
Katika taarifa hiyo, ilielezwa kuwa EU itaendelea kuratibu msimamo huu na washirika wake.
Taarifa hiyo ambayo ilisema kwamba EU "inaelezea mshikamano kamili na nchi wanachama Czechia na Marekani", pia ilitoa wito kwa Urusi iheshimu kabisa Mkataba wa Vienna.
Serikali ya Urusi ilitangaza kwamba imeidhinisha orodha ya "nchi zenye uhasama" zilizoandaliwa kwa kuzingatia mitazamo ya nchi zingine kuelekea Moscow, na Marekani na Czechia zilijumuishwa kwenye orodha hiyo.

No comments:
Post a Comment