Search This Blog

Monday, May 17, 2021

Jumuiya ya Ulaya yakosoa orodha ya nchi zenye uhasama iliyochapishwa na Urusi


Jumuiya ya Ulaya (EU) ilikosoa vikali uchapishaji wa orodha ya "nchi zenye uhasama" na Urusi.

Kulingana na ripoti ya Sputnik, Josep Borrell, Mwakilishi Mkuu wa EU wa Maswala ya Kigeni na Sera ya Usalama, alitaka kutafakariwa tena kwa uamuzi huu ili kuzuia kuzorota zaidi kwa uhusiano "uliodhoofishwa."

Katika taarifa hiyo, ilielezwa kuwa EU itaendelea kuratibu msimamo huu na washirika wake.

Taarifa hiyo ambayo ilisema kwamba EU "inaelezea mshikamano kamili na nchi wanachama Czechia na Marekani", pia ilitoa wito kwa Urusi iheshimu kabisa Mkataba wa Vienna.

Serikali ya Urusi ilitangaza kwamba imeidhinisha orodha ya "nchi zenye uhasama" zilizoandaliwa kwa kuzingatia mitazamo ya nchi zingine kuelekea Moscow, na Marekani na Czechia zilijumuishwa kwenye orodha hiyo.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...