Search This Blog

Wednesday, May 19, 2021

Jumuiya ya Kimataifa yaombwa kuokoa uchumi wa Afrika


Rais Samia Suluhu Hassan leo ameshiriki kwa njia ya mtandao kwenye mkutano wa Wakuu wa nchi na mashirika ya Kimataifa uliojadili namna ya kuokoa uchumi wa nchi za Afrika kufuatia madhara yaliyosababishwa na ugonjwa wa corona.

Mkutano huo uliofanyika jijini Paris, -Ufaransa uliandaliwa na Rais Emmanuel Macron wa nchi hiyo na kuhudhuriwa na Marais wa nchi za Angola, Burkina Faso, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Ivory Coast, Misri, Ethiopia, Ghana, Mali, Mauritania, Msumbiji, Nigeria, Rwanda, Senegal, Sudan, Togo, Tunisia, Italia, Hispania na Umoja wa Ulaya.

Marais wa Tanzania, Kenya, Afrika Kusini, Uholanzi, Ujerumani, China na Japan wameshiriki kwenye mkutano huo wa njia ya mtandao. 

Mashirika ya Kimataifa yaliyoshiriki ni Umoja wa Mataifa, Shirika la Fedha la Kimataifa, Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo Duniani, Shirika la Biashara Duniani na Benki ya Dunia.

Wakati wa mkutano huo, Rais Samia Suluhu Hassan ameungana na Marais wengine duniani kumpongeza Rais Macron kwa kuitisha mkutano huo, ambao wamesema umelenga sio tu kusaidia uchumi wa Bara la Afrika bali kuokoa maisha ya binadamu waliopo Afrika kutokana na kuathirika na madhara yaliyosababishwa na corona.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...