Search This Blog

Monday, May 31, 2021

Israel yakaribia kupata serikali mpya bila Netanyahu


Mwanasiasa anayependelea sera za kizalendo nchini Israel Naftali Bennet amesema jana kuwa atajiunga na juhudi za kuunda serikali ya muungano itakayomuondoa madarakani waziri mkuu Benjamin Netanyahu. 

Akizungumza baada ya kukutana na wajumbe wa chama chake cha Yamina, Bennet amesema atafanya kila linalowezekana kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na kiongozi wa upinzani nchini humo Yair Lapid.

 Lapid ana muda wa hadi Jumatano inayokuja kufanikisha uundaji wa muungano wa vyama utakaokuwa na wingi wa viti bungeni kumwezesha kuunda serikali mpya. 

Wabunge wa Israel wanaompinga waziri mkuu Netanyahu na chama chake cha Likud wamekuwa kwenye majadiliano mazito ya kuunda muungano baada ya uchaguzi wa mwezi Machi kushindwa kutoa mshindi wa moja kwa moja wa kuunda serikali.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...