Search This Blog

Monday, May 17, 2021

Dkt. Florence Samizi atangazwa mshindi wa Ubunge jimbo la Muhambwe


Uchaguzi mdogo katika majimbo mawili ya Muhambwe na Buhigwe yote ya mkoani Kigoma, ambao ulifanya Mei 16, 2021 umemalizika kwa Chama Cha Mapinduzi kuibuka na ushindi katika majimbo yote.

Mshindi wa uchaguzi mdogo wa ubunge, jimbo la Muhambwe kupitia CCM, Dkt. Florence Samizi.

Msimamizi wa uchaguzi wa ubunge Jimbo la Muhambwe, Bw. Diocles Rutema amemtangaza mgombea wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Florence Samizi kuwa mshindi wa kiti hicho kwa kupata kura 23,441.

Aliyefuatia ni mgombea wa ACT Wazalendo Bw. Masabo Julius aliyepata kura 10,847 na Mgombea wa Democratic Party (DP), Bw. Philipo Fumbo aliyepata kura 368.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...