Search This Blog

Wednesday, May 26, 2021

Baraza la Usamala la UN kufanya mkutano juu ya Mali


Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kufanya mkutano wa dharura na wa faragha kuhusu Mali hii leo, baada ya jeshi la nchi hiyo kuwakamata viongozi wawili wa serikali ya mpito. 

Mkutano huo umependekezwa na Ufaransa, Niger, Tunisia, Kenya pamoja na Saint Vincent na Grenadines. Kanali Assimi Goita amesema jana kwamba amemuondoa madarakani rais wa mpito na waziri mkuu, waliopewa jukumu la kurejesha tena utawala wa kiraia baada ya mapinduzi ya Agosti iliyopita.

 Hatua yake hiyo imelaaniwa vikali na jumuiya ya kimataifa iliyotoa vitisho vya kuiwekewa Mali vikwazo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...