Mtayarishaji mkongwe wa video za muziki nchini Adam Juma amewasihi wasanii wa muziki haswa chipukizi kuzingatia sana kupeleka kazi zao redioni hata kama za mtaani maana huko ndiko kwenye mashabiki wa kweli walipo kuliko kutegemea views YouTube.
Adam amefunguka kuwa kuna level wasanii wakubwa wanaweza wakajidai kwa kutumia YouTube views lakini kwa hawa wachanga ni hatari maana kuwa na YouTube views nyingi hazimaanishi kuwa nyimbo yako ndio imehit mtaani.
"Kuna wengine hili swala la views ni biashara na inawalipa, views nyingi zinamlipa zaidi na haoni tabu kuinvest kwenye kuongeza kwa sababu soko lake linamruhusu kufanya hivyo".
Adam Juma ametoa maoni yake kuhusu ishu ya views inayoendelea kwa sasa.

No comments:
Post a Comment