Waziri Mkuu wa Armenia Nikol Pashinyan ametangaza kwamba amejiuzulu kabla ya uchaguzi wa mapema utakaofanyika nchini humo.
Pashinyan, katika ujumbe wake kwenye ukurasa wake wa Facebook, alisema,
"Nimejiuzulu kama waziri mkuu leo kufanya uchaguzi wa mapema wa bunge mnamo Juni 20, kulingana na makubaliano yaliyofikiwa na rais na vikosi vya kisiasa nchini."
Pashinyan amesema kuwa ataendelea na majukumu yake kama waziri mkuu kwa muda.
Pashinyan amesema kuwa atashiriki katika uchaguzi wa mapema kama mgombea wa waziri mkuu wa Mkataba wake wa Kiraia, ambao ni sehemu ya Muungano wa sasa.
Toka Armenia ishindwe katika ya vita vya Nagorno-Karabakh dhidi ya Azerbaijan, mivutano ya kisiasa imekuwa ikiongezeka nchini humo na hivyo kupelekea kufanyika kwa uchaguzi wa mapema.
Uchaguzi unatarajiwa kufanyika Juni 20.
Pashinyan alisema mapema, "Nitajiuzulu Aprili. Lakini nitafanya hivyo sio kuondoka mamlakani, lakini kufanya uchaguzi wa mapema."

No comments:
Post a Comment