Search This Blog

Wednesday, April 7, 2021

Tetesi za soka kimataifa

 


West Ham itafanya vyovyote vile ili kumnasa kiungo wa kati Jesse Lingard, 28, anayekipiga Manchester United. (Sky Sports)

Thamani ya Lingard kwa mujibu wa Manchester United ni pauni milioni 30. (Mirror)

Arsenal imerejesha nia yao tena kwa mshambuliaji wa Crystal Palace Wilfried Zaha,28. (90min)

Manchester City wanalenga kukubaliana kuingia mkataba mpya nawashambuliaji wa England Phil Foden,20, na Raheem Sterling,26, kabla ya mwishoni mwa msimu, baada ya kiungo wa kati wa Ubelgiji Kevin de Bruyne,29, kuongeza mkataba wake wa mpaka mwaka 2025. (Eurosport)

Manchester City haitamfuatilia mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi mpaka mchezaji huyo, 33, atakapoweka wazi kuwa anataka kuondoka Barcelona. (Marca-in Spanish)

Chelsea wanajiandaa kutoa ofa ya pauni milioni 86.3 kwa ajili ya mshambuliaji Mbelgiji anayecheza katika klabu ya Inter Milan Romelu Lukaku, 27, endapo the Blues watashindwa kumsajili mshambuliaji Erling Braut Haaland,20, wa Borussia Dortmund (Calciomercato-in Italian)

Tottenham watajaribu kumsajili mlinzi wa kati wa Southampton Jannik Vestergaard,28, mwenya thamani ya pauni milioni 18, baada ya dirisha la usajili kufunguliwa. (Express)

Liverpool wameiambia RB Leipzig kuwa hawatamsajili mlinzi wa kati, Mfaransa Ibrahima Konate,21, (Bild, via Express)

Reds watakabiliwa na ushindani wa Chelsea katika kumnasa kiungo wa kati wa Ajax Ryan Gravenberch,18, ambaye anatazamwa kuwa mbadala wa Georginio Wijnaldum,30. (Gazzetta dello Sport,via Express)

Simba yatinga Robo Fainali Afrika kwa kishindo, barakoa za mashabiki zawa gumzo

Kocha wa zamani wa Bournemouth anamtaka mshambuliaji wa Everton Josh King,29, kuwa mchezaji wa kwanza kumsajili akiwa kocha wa Celtic. (Sun)

Barcelona wanataka kuongeza mkataba wa mshambuliaji wa Kifaransa Ousmane Dembele mpaka mwaka 2025. Klabu hiyo ya La Liga inamtaka mchezaji huyo mwenye miaka 23 ambaye mkataba huo unamalizika mwaka 2022- apatikane katika soko la usajili iwapo makubaliano hayatafikiwa. (Sport-in Spanish)

Barcelona wameendelea kumfuatilia mlinzi wa Manchester City, Mhispania Eric Garcia lakini wametoa ofa pungufu ikilinganishwa na iliyowekwa mezani mwaka jana uliopita. (Marca)

Bayern Munich imethibitisha kuwa mlinzi wa Kijerumani Jerome Boateng, 32, ataondoka kwenye klabu hiyo baada ya mkataba wake kumalizika msimu huu. (Sky Sports, via Goal)

Southamp na West Ham ni miongoni mwa vilabu vinavyovutiwa na kiungo wa kati wa Manchester City Yangel Herrera,23, ambaye anacheza kwa mkopo katika klabu ya Granada. (Goal)

Kocha wa Arsenal Mikel Arteta anamtaka Lucas Torreira kuwa na subira baada ya kiungo wa kati wa Uruguay,25, ambaye anacheza kwa mkopo Atletico Madrid, kuomba kuwaacha washika bunduki hao kwenda Boca Juniors. (Mirror)



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...