Somalia imepokea dozi 200,000 za chanjo ya Sinopharm Covid-19 kutoka Uchina.
Waziri wa afya Fawziya Abikar alipokea dozi hizo kutoka kwa balozi wa Uchina nchini Somalia Qin Jian.
Wizara ya afya ya nchi hiyo ilituma picha za tukio hilo kwenye mtandao wake wa Twitter:
Somalia ilikuwa imepokea shehena ya kwanza ya dozi 300,000 za chanjo kupitia mpango wa Covax.
Jumla ya watu 12,406 walithibitishwa kupatwa na maambukizi ya virusi vya corona ikiwa ni pamoja na vifo 618, kulingana na takwimu kutoka wizara ya afya nchini humo.

No comments:
Post a Comment