Serikali ya Japan itatoa msaada wa kifedha wa jumla ya dola milioni 39 kwa ajili ya mtandao wa usambazaji wa minyororo ya hifadhi baridi ya chanjo ya corona (Covid-19) kwa nchi 31.
Kulingana na taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje, msaada wa kifedha utakaotolewa kwa nchi za Afrika, Amerika Kusini na Caribbean kupitia Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), itatumika katika kuanzisha vituo vya uhifadhi baridi kwa ajili ya chanjo na vifaa vya usafirishaji.
Miongoni mwa nchi ambazo zitafaidika na msaada huo ni Guatemala, Haiti, Jamaica, Nicaragua, Paraguay, Venezuela, Misri, Ethiopia, Nigeria, Libya na Tunisia.
Akitaja umuhimu wa usambazaji wa chanjo katika mkutano wake na waandishi wa habari, Waziri wa Mambo ya Nje Motegi Toshimitsu alisema,
"Tunataka kuendelea na msaada wetu kwa kutumia nguvu ya Japan."
Japan pia iliahidi dola milioni 200 kwa Programu ya Usambazaji Chanjo ya Covid-19 (COVAX), ambayo inakusudia kutoa dozi bilioni 2 za chanjo ya Covid-19 kote ulimwenguni ifikapo mwishoni mwa 2021.

No comments:
Post a Comment