Kitendo cha kumwagiwa tindikali usoni mwa mwanafunzi wa chuo kikuu mwenye asili ya Pakistan katika mkoa wa Long Island jimbo la New York nchini Marekani (USA), kilizua mijadala ya chuki dhidi ya Waislamu kama ajenda kuu.
Katika mahojiano na idhaa ya WCBS, Nafiah Ikram (21) alisema kwamba alishambuliwa kwa tindikali na mtu asiyejulikana wakati alipokuwa akielekea nyumbani kwake Elmont.
Akibainisha kwamba alikuwa amelazwa hospitalini kwa wiki 3 baada ya shambulizi hilo, Ikram alisema kuwa tindikali hiyo ilisababisha kuteketea uso, macho, shingo na mikono.
Ikram alisema, "Maisha yangu yote yamebadilika ndani ya dakika 5. Ninaweza kuchagua rangi tu hivi sasa. Nataka kufahamu ni nini hasa sababu ya shambulizi hili. Kwani nimefanya nini mpaka kustahili kufanyiwa hivi?"
Baraza la New York la Uhusiano wa Marekani na Uisilamu (CAIR) limetaka mhusika akamatwe haraka iwezekanavyo na kuchunguza shambulizi hilo kama uhalifu wa chuki dhidi ya Waislamu.
Idara ya Polisi ya Wilaya ya Nassau iliwataka raia kutoa taarifa kwa kuweka zawadi ya dola elfu 10 ili kumkamata mshambuliaji ambaye alitoroka baada ya tukio hilo.

No comments:
Post a Comment