Maafisa wa Indonesia wametangaza kuwa wafanyakazi 53 waliokuwa ndani ya manowari iliyopotea nchini mnamo Aprili 21, walifariki.
Marshal Hadi Tjahjanto, Kamanda wa Kikosi cha Jeshi la Kitaifa la Indonesia, alisema katika taarifa kuwa kuna ushahidi wazi kwamba manowari hiyo haikutoweka, bali ilizama karibu na Kisiwa cha Bali.
Kwa upande mwingine, maafisa wa jeshi walitangaza kwamba akiba ya oksijeni ya manowari ilikuwa imekwisha mapema leo hii na wanatumai kuwa wafanyikazi wa manowari hiyo bado watakuwa hai.
Manowari hiyo ya KRI Nanggala-402 ilipotea baada ya kupoteza mawasiliano mnamo Aprili 21.
Ilitangazwa kwamba manowari hiyo ilipotea kilomita 95 kaskazini mwa Kisiwa cha Bali.
Jeshi la Wanamaji la Indonesia lilituma meli 6 za kivita, helikopta 1 na wafanyikazi 400 katika mkoa huo kutafuta manowari iliyopotea.

No comments:
Post a Comment