Search This Blog

Thursday, April 22, 2021

David Alaba akubali kujiunga na Real Madrid

 


Mlinzi wa Bayern Munich, David Alaba amefikia makubaliano ya kujiunga na klabu ya Real Madrid ifikapo wakati wa majira ya kiangazi msimu huu.

Alaba atasaini mkataba wa miaka mitano na Los Blancos ambao utamuweka nchini Hispania hadi majira ya joto ya mwaka 2026.

Taarifa hii inamalizia sakata la muda mrefu juu ya hatma ya nyota huyo ambaye mapema mwaka huu alithibitisha kuwa angeondoka nchini Ujerumani lakini haikufahamika angejiunga na klabu ipi.

Nyota huyo raia w Australia ambaye ameitumikia The Bavarians kwa takribani miaka 13 kwa mafanikio, alikuwa akihusishwa kwa muda mrefu sasa na kuhamia nchini Hispania huku Barcelona nayo ilikuwa ikiwania saini yake.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...