Mahakama ya Ufaransa inatarajiwa kutoa uamuzi wake katika kesi ya ufisadi inayomkabili rais wa zamani Nicolas Sarkozy leo Jumatatu, huku waendesha mashtaka wakishinikiza muda zaidi gerezani kwa kiongozi huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 66.
Sarkozy ambaye aliiongoza Ufaransa kutoka mwaka 2007 hadi mwaka 2012, anatuhumiwa kutoa nafasi ya kazi kwa jaji mmoja mjini Monaco kwa sharti kuwa angepata habari zaidi kuhusu uchunguzi juu ya fedha zake za kampeni.
Rais huyo wa zamani ameiambia mahakama kuwa "hajawahi kufanya vitendo vyovyote vya ufisadi." Waendesha mashtaka wanataka apewe kifungo cha miaka minne jela na kutumikia angalau miaka miwili, na pia wanataka adhabu kama hiyo kwa washtakiwa wenzake-wakili Thierry Herzog na jaji Gilbert Azibert.

No comments:
Post a Comment