Search This Blog

Monday, March 1, 2021

Okonjo-Iweala aanza rasmi kazi kama mkuu wa WTO


Dkt Okonjo-Iweala ni mwanamke wa kwanza Mwafrika kushikilia nafasi hiyoImage caption: Dkt Okonjo-Iweala ni mwanamke wa kwanza Mwafrika kushikilia nafasi hiyo

Mnageria-Mmarekani, Ngozi Okonjo-Iweala, anaanza rasmi kazi kama mkuu mpya wa Shirika la Biahsara Duniani (WTO) Jumatatu ya leo.

Dkt Okonjo -Iwela ambaye ni waziri wa zamani wa fedha na mambo ya nje wa Nigeria, ni mwanamke wa kwanza wa Afrika kuongoza WTO.

Ngozi Okonjo-Iweala amesema kipaumbele chake ni kushughulikia masuala ya afya na athari za kiuchumi zinazotokana na majanga.

Kuna wasiwasi huko Washington na miji mikuu mingine kuhusu sera za biashara za China na jinsi WTO inavyojiandaa kushughulikia masuala hayo.

Dkt Okonjo-Iweala anafahamika kwa kuwa mwana -mageuzi, lakini atakabiliwa na mslahi ya nchi wanachama.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...