Search This Blog

Thursday, February 11, 2021

Yanga kuanza safari leo kuwafuata Mbeya City


 KIKOSI cha Yanga leo kinatarajia kuanza safari kuelekea Mbeya kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mbeya City. 

Mchezo huo wa mzunguko wa pili unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Sokoine, Mbeya ambapo Yanga wamewaomba mashabiki wao wajitokeze kwa wingi kuwapokea leo mchana Uwanja wa ndege wa Songwe, Mbeya.

Walipokutana Uwanja wa Mkapa, Yanga ilisepa na pointi tatu muhimu kwenye mzunguko wa kwanza baada ya kushinda bao 1-0 lililopachikwa na Lamine Moro. 

Februari 13 watakutana uwanjani wakiwa na mtambo wao wa mabao Fiston Abdulazack ambaye ni ingizo jipya ndani ya vinara hao wa Ligi Kuu Bara wakiwa na pointi 44.

Cedric Kaze, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa wapo tayari kwa mchezo huo na watapambana kupata matokeo chanya.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...