Watu 23 wameripotiwa kupoteza maisha baada ya kushambuliwa na watu waliojihami kwa silaha nchini Nigeria.
Kamishna wa Usalama na Mambo ya Ndani wa Mkoa wa Kaduna, Samuel Aruwan, , alitoa maelezo na kuarifu kwamba washambuliaji wenye silaha ambao bado hawajafahamika waliendesha mashambulizi katika maeneo ya Birnin Gwari, Giwa, Chikun, Igabi na Kauru mkoani humo.
Aruwan alibainisha kuwa watu 23 walipoteza maisha na wengine wengi walijeruhiwa kwenye mashambulizi hayo.
Akifahamisha kuwa vikosi zaidi vya usalama vimetumwa mkoani humo kutokana na kuongezeka kwa mashambulizi, Aruwan pia alisema kuwa uchunguzi umeanzishwa kuhusiana na tukio hilo.

No comments:
Post a Comment