Search This Blog

Wednesday, February 3, 2021

Watoto watano washambuliwa na kuuawa Marekani


Watu sita, 5 kati yao watoto, wameariki katika shambulizi la kutumia silaha katika nyumba moja katika mji wa Muskogee katika jimbo la Oklahoma la Marekani.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na polisi, timu za polisi zilifika eneo la tukio kwa sababu ya kusikia milio ya risasi kutoka nyumba. Polisi walimkamata mshukiwa aliyekuwa akitaka kutoroka.

Imeelezwa kuwa watu 5, 4 kati yao watoto, walipatikana wakiwa wamepoteza maisha ndani ya nyumba hiyo.

Mtoto mmoja na mwanamke walipelekwa hospitalini wakiwa na majeraha.

Walakini, iliripotiwa kuwa mtoto huyo alifariki hospitalini, na mwanamke huyo bado yupo katika hali mbaya.

Polisi hawajazungumza lolote kuhusu nani aliyehusika na shambulizi hilo la kinyama.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...