Vikosi vya usalama dhidi ya waandamanaji vimeongezwa kutokana na athari ya maandamano yaliyoendelea baada ya mapinduzi ya kijeshi na kuwekwa kizuizini kwa wanachama wa serikali nchini Myanmar.
Katika taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa wa Facebook wa jeshi la Myanmar, ilitangazwa kwamba sheria ambayo ilihitaji agizo la mahakama kwa vikosi vya usalama kuwazuilia washukiwa, ilisitishwa kwa muda.
Kwa kuongezea, raia walilazimika kuripoti kwa polisi ziara zao za nyumbani za usiku wa manane.
Wakati huo huo, maandamano ya mapinduzi dhidi ya jeshi yaliendelea siku ya 8 katika miji mikubwa ya nchi hiyo.
Katika mji mkuu wa Nepido, kundi la waandamanaji wanaopinga mapinduzi walipinga utawala wa jeshi kwa kupiga kelele za honi za magari yao.
Na katika jiji la Yangon ambalo lina watu wengi zaidi nchini humo, wanafunzi wa vyuo vikuu walibeba mabango na picha za Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje na kiongozi halali wa nchi hiyo, Aung San Suu Kyii, ambao walizuiliwa kabla ya mapinduzi, wakiwataka viongozi hao kuachiliwa huru.
No comments:
Post a Comment