KATIKA kuadhimisha miaka 44 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Dodoma Mjini umekabidhi misaada yenye thamani ya Sh. Milioni Moja kwa watoto wenye ulemavu wa akili na kuwatembelea wakina mama waliojifungua katika Hospitali ya Mkoa.
Misada iliyotolewa ni pamoja na Juisi, Mchele, Pipi, Sukari, Mafuta ya kupaka, Miswaki na Madaftari
Akizungumza mara baada ya kukabidhi misaada hiyo Katibu wa UWT Wilaya ya Dodoma Mjini, Diana Madukwa amesema wameamua kufanya mambo yanayogusa jamii pamoja na kuwatembelea ili kujua changamoto zinazowakabili na kuyafikisha mahali panapohusika.
“Katika kuadhimisha miaka 44 ya kuzaliwa kwa CCM tumeamua kwenda kutembelea watoto ambao wana ulemavu wa akili na kuwapa msaada wakina mama ambao wamejifungua katika hospitali ya mkoa wa Dodoma kwasababu ni maeneo ambayo yanayogusa jamii moja kwa moja," Amesema Madukwa.
Madukwa ameiasa jamii kuwa na tabia ya kusaidia watoto waishio katika mazingira hatarishi na na wenye mahitaji maalumu huku akisisitiza jamii kuacha tabia ya kuwanyanyapaa kundi hilo kwani nao ni binadamu.
Amesema CCM ni chama tawala kinagusa kila tabaka na kuhakikisha kila mtu ambaye amezaliwa katika ardhi ya Tanzania anapata haki zake kulingana na maumbile yake.

No comments:
Post a Comment