Search This Blog

Thursday, February 25, 2021

UN yatoa wito kwa vyama vya kisiasa vya Somalia


Umoja wa Mataifa (UN) uliripoti kwamba vyama vyote vya kisiasa nchini Somalia vinapaswa kuhakikisha usalama wa raia.

Ofisi ya Uratibu wa Masuala ya Kibinadamu ya UN (UNOCHA) ilisisitiza katika taarifa yake kwenye Twitter kwamba mashirika ya misaada yana wasiwasi kuwa mzozo wa silaha utazidisha hali mbaya ya kibinadamu nchini.

Taarifa hiyo ambayo iliambatana na maelezo yaliyosema "Mvutano wa kisiasa nchini Somalia huenda ukaathiri maisha ya watu,"  pia ilionya na kusisitiza kwamba vyama vyote vya kisiasa lazima vihakikishe usalama wa raia.

Mvutano kati ya utawala wa Mogadishu na upinzani unaendelea nchini Somalia kutokana na kushindwa kutekeleza uchaguzi wa urais mnamo tarehe 8 Februari.

Rais Mohammed Abdullah Farmaju alisema kuwa uchaguzi hauwezi kufanyika katika tarehe iliyopangwa kwa madai kukosekana makubaliano juu ya kanuni na upinzani, na kudai kwamba Rais hakutaka kurithisha madaraka yake.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...