Search This Blog

Saturday, February 27, 2021

Seth, Rugemalira na siku 1349 mahabusu

 


Wafanyabiashara wawili maarufu nchini Tanzania, Harbinder Sethi na James Rugemalira wanaokabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi, wakituhumiwa kujipatia fedha  katika akaunti ya Tegeta Escrow wana siku 1349 mahabusu sawa na miaka mitatu, miezi nane na siku nane hadi leo Jumamosi Februari 27, 2021.


Wapo mahabusu kwa kuwa wanakabiliwa  na mashtaka yasiyodhaminika, huku upelelezi wa kesi yao ukiwa haujakamilika.


Seth na Rugemalira walifikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Juni 19, 2017 wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 27/2027 yenye mashtaka 12.


Ukiwaona wawili hawa walivyo sasa ni tofauti na siku ya kwanza walivyofikishwa mahakamani kwa sababu kwa nyakati tofauti walikumbana na changamoto mbalimbali.


Desemba 20, 2019 aliongezeka mshatakiwa katika kesi hiyo ambaye ni aliyekuwa mwanasheria wa kampuni ya  kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Joseph Makandege na alifikishwa mahakamani akikabiliwa na mashtaka matano likiwemo la kuisababishia hasara Serikali ya dola 980,000.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...