Search This Blog

Wednesday, February 10, 2021

Rais wa Somalia aitisha mkutano kutatua mgogoro


Rais wa Somalia Mohamed Abdullahi Farmajo ameitisha mkutano na viongozi wa serikali ya shirikisho wiki ijayo ili kutatua mkwamo wa jinsi ya kuendelea na uchaguzi.

Muhula wa Rais Farmajo ulimalizika Jumatatu baada ya mazungumzo kuhusu uchaguzi kuvunjika mnamo tarehe 5 Februari.

Vikundi vya upinzani vimesema havitambui tena mamlaka ya Bwana Farmajo na walitaka kuundwa kwa ushirika wa mpito.

Ofisi ya rais iliandika katika ukurasa wa twitter kuhusu mkutano uliopangwa kufanyika wiki ijayo huko Garowe, jimbo la Puntland.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jumanne liliwahimiza viongozi wa Somalia "kufikia makubaliano ya kufanyika kwa uchaguzi.

Limekaribisha kutangazwa kwa mazungumzo zaidi tarehe 15 Februari.

Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat Jumatatu alikuwa amemtaka Rais Farmajo na viongozi wa serikali ya shirikisho "kufikia makubaliano juu ya maswala yaliyosalia ili kuruhusu kufanyika kwa uchaguzi wa bunge na urais bila kuchelewa sana".






No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...