Search This Blog

Thursday, February 18, 2021

Raia wa Libya washerehekea Maadhimisho ya Miaka 10 ya Mapinduzi


Raia wa Libya, wanasherehekea miaka 10 ya Mapinduzi ya Februari 17 mwaka 2011, ambayo yalimaliza utawala wa miaka 42 wa Muammar Gaddafi.

Wananchi wa Libya hushiriki katika sherehe kwenye mitaa na viwanja mbalimbali kote nchini, katika miji ya Misrata, Zawiya, Zintan, Sebha na mji mkuu wa Tripoli.

Katika kipindi cha maadhimisho ya miaka 10 ya mapinduzi, siku za Februari 17 na 18 zilitangazwa likizo rasmi, wakati barabara na viwanja vilikuwa vimepambwa kwa bendera za Libya.

Wananchi wengi waliojaza eneo la wazi la umma la Mashujaa wa Tripoli waliongozana kwa nyimbo za mapinduzi na bendera zao.

Sherehe rasmi haikufanyika Benghazi ambao ni mji wa pili kwa ukubwa nchini, ambapo pia uliandaa Mapinduzi ya Februari 17 kama eneo la maandamano ya kwanza dhidi ya utawala wa Muammar Gaddafi.

Mji wa Benghazi ambao una Baraza la Kitaifa la Serikali ya Mpito, ulikuwa wa kwanza kukombolewa kutoka kwa vikosi vya Gaddafi mnamo 2011 na kupinga serikali ya kwa mara ya kwanza na baadaye kuanzishwa vikosi vya wanamgambo wa jenerali mstaafu Khalifa Haftar ambaye anataka kuchukua nchi kwa mapinduzi.

Sherehe za mapinduzi zilizuiwa katika mji wa Sebha, eneo la Fezzan, mkoa wa kusini mwa Libya,  

Mtoto mmoja aliuawa na zaidi ya watu 10 walijeruhiwa katika shambulizi la roketi lililolenga wale waliohudhuria sherehe hiyo.

Ubalozi wa Uturuki nchini Libya ulituma ujumbe wa pongezi wa maadhimisho ya mapinduzi.

Taarifa zifuatazo zilijumuishwa katika ujumbe wa ubalozi:

"Tunawapongeza ndugu zetu wa Libya katika Maadhimisho ya Miaka 10 ya Mapinduzi ya Februari 17. Tunataka kuhakikisha utulivu na ustawi nchini Libya. Uturuki itakuwa karibu katika mchakato wa Libya na wananchi wake kwa ujumla."




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...