Search This Blog

Tuesday, February 23, 2021

Raia wa Korea Kaskazini aingia eneo la kijeshi la Korea Kusini mfumo wao wa kiusalama ukionesha hitilafu


Vikosi vya Korea Kusini vimeshindwa kumgundua mwanamume wa Korea Kaskazini aliyevuka mpaka na kuingia upende wa Korea Kusini unaolindwa vikali mwezi huu hata baada ya kuonekana kwenye kamera za televisheni mara nane na kuzua taharuki.

Jeshi la Korea Kusini limesema litachukulia tukio hilo kama hitaji la kufanyika mabadiliko ya kiusalama haraka iwezekanavyo.

Mwanamume huyo aliogelea na kutoka baharini akiwa na suti yenye maji, na kutembea umbali wa kilomita 5 na kuwa katika eneo hilo kwa saa tatu bila kugundulika kabla ya wanajeshi hatimaye kuchukua hatua alipojitokeza kwa mara ya 9.

Bado haijafahamika kwanini aliamua kuvuka katika eneo hatari namna hiyo.

Kuna wakati mwanamume huyo alipita katika handaki kwenye eneo lisiloruhusiwa shughuli za kijeshi na jeshi la Korea Kusini halikubaini lolote wakati huo, shirika la habari la Yonhap limesema.

Ni kwanini Korea iligawanyika?

Tangu kugawanyika kwa Korea mbili baada ya Vita kuu ya pili ya dunia, Korea Kaskazini na Korea Kusini zimekuwa na utofauti mkubwa wa utajiri

Hii ni licha ya eneo hilo kuwa moja ya yanayolindwa vikali duniani na lenye ving'amuzi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...