Search This Blog

Saturday, February 6, 2021

Mtanzania Himid Mao ‘Ninja’ amekamilisha dili la kujiunga na Entag El Harby FC ya Misri


 KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania, Himid Mao ‘Ninja’ amekamilisha dili la kujiunga na Entag El Harby FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Misri akitokea Enppi FC.

Himid amejiunga na klabu hiyo akiwa mchezaji huru, kufuatia mkataba wake na Enppi kufikia kikomo mwishoni mwa msimu uliopita.Himid anakuwa mchezaji wanne kusajiliwa na Entag El-Harby SC akitanguliwa na Ahmed Saber pia kutoka Enppi, Mohamed Sosta kutoka Aswan na kipa Ahmed Busca.

Entag El-Harby SC imekuwa na mwanzo mbaya katika msimu huu, hali iliyosababisha kuburuza mkia kwenye msimamo wa ligi hiyo, ikiwa na alama tano tu, baada ya kucheza michezo tisa, hivyo kusababisha kocha mkuu wa timu hiyo, Mokhtar Mokhtar kutimuliwa kazi.

Himid Mao alianza kucheza soka Misri mnamo Julai 2018, akisajiliwa na Petrojet, lakini mwaka mmoja baadaye alihamia Enppi, akiichezea michezo 22 msimu uliopita.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...