Search This Blog

Saturday, February 13, 2021

Mawakili wa Trump wayataja mashtaka kama kisasi cha kisiasa


Timu ya mawakili wa rais wa zamani wa Marekani Donald Trump, imeutaja mchakato wa mashtaka dhidi ya Mrepublican huyo kama kisasi cha Wademocrat.

 Mwanasheria Michael van der Veen, alisema mwanzoni mwa kuwasilisha hoja za utetezi mbele ya baraza la Seneti kwamba Trump hakuamuru vurugu katika hotuba yake aliyoitoa muda mfupi kabla ya uvamizi wa bunge Januari 6. 

Waendesha mashtaka wa chama cha Democratic walikamilisha ushahidi wao dhidi ya Trump siku ya Alhamisi. 

Walihoji kuwa rais huyo wa zamani anawajibika moja kwa moja kwa uvamizi wa makao ya bunge, maarufu kama Capitol, na kulisihi baraza la seneti kumtia hatiani kwa kuchochea machafuko.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...