Search This Blog

Friday, February 26, 2021

Marekani ipo ''kwenye mazungumzo'' kuhusu kesi ya Rusesabagina


Kesi ya Paul Rusesabagina, mfanyakazi wa hoteli aliyeitwa shujaa kwenye filamu ya Hollywood kuhusu mauaji ya kimbari nchini Rwanda, Hotel Rwanda, inaanza leo.

Anashtakiwa kwa makosa ya ugaidi, mauaji na uhalifu mwingine. Mawakili wake wamekana mashtaka hayo dhidi yake.

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani ilisema siku ya Alhamisi kuwa

imeshirikiana na serikali ya Rwanda katika "kwa kiasi kikubwa" huko "Washington na pia Kigali".

‘’Tunaamini mchakato wa kisheria utakuwa wa haki na uwazi, utakaoheshimu utawala wa sheria, na unaokwenda sawa na kuwajibika kwa Rwanda katika kuheshima haki za kimataifa za binadamu. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya nje Ned Price aliwaambia waandishi wa habari.

Bwana Rusesabagina ni mkosoaji mkubwa wa Rais Paul Kagame, na amekuwa akiishi uhamishoni nchini Marekani.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...