Search This Blog

Friday, February 5, 2021

Maandamano yamefanyika Indonesia ili kupinga mapinduzi ya jeshi Myanmar


Kikundi kidogo kilichokusanyika mbele ya Ubalozi wa Myanmar huko Jakarta katika mji mkuu wa Indonesia, kilipiga kelele kauli za kupinga mapinduzi na kuunga mkono demokrasia nchini Myanmar.

Kundi hilo, lililobeba mabango ya "Tuko pamoja na watu wa Myanmar", "Demokrasia ya Myanmar" na "Amani nchini Myanmar" lilitaka mapinduzi kusitishwa.

Mvutano uliongezeka nchini Myanmar juu ya madai ya udanganyifu katika kuhesabu kura kwenye uchaguzi mnamo tarehe 8 Novemba 2020.

Jeshi la Myanmar lilitwaa madaraka tarehe 1 Februari, hali ya hatari ilitangazwa kwa mwaka 1, Rais Win Myint, Waziri wa Mambo ya nje na kiongozi wa chama cha nchi hiyo Aung San Suu Kyi na viongozi wakuu wa chama tawala cha NLD walikamatwa.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...