Search This Blog

Thursday, February 25, 2021

Kituo cha wapenzi wa jinsia moja chafungwa Accra Ghana


Polisi nchini Ghana wamefunga kituo cha kuwahudumia wapenzi wa jinsia moja ambacho kilifunguliwa hivi karibuni katika mji mkuu wa Accra, kufuatia malalamishi ya umma.

"Hatuwezi tena kufikia eneo letu salama na usalama wetu unatishiwa. tunomba mashirika ya kutetea haki za binadamu, na washirika wao kuangazia shambulio hili na uhalifu wa chuki tunaotendewa," Wanaharakati wa kutete haki za wapenzi wa jinsia moja nchini Ghana walisema kwenye mtandao wa Twitter.

Makundi ya kutetea haki, ikiwemo Muungano wa Haki sahihi za Kijinsia, Binadamu na Maadili ya Familia pamoja na Kongamano la Maaskofu wa katoliki Ghana (GCBC), yamekuwa yakishinikiza serikali kufunga kituo hicho.

Kilifunguliwa kupitia hafla ya mchango wa fedha uliohudhuriwa na wanadiplomasia kadhaa wa Muungano wa Ulaya (EU) na wakigeni.

Picha za kufunguliwa kwa kituo hicho zilizosambazwa katika mitandao ya kijamii zimezua hisia mseto.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...