Search This Blog

Wednesday, February 24, 2021

Kagame ataja 'unafiki' katika usambazaji wa chanjo ya corona


Rais wa Rwanda Paul Kagame amesema kuna "unafiki" katika usambazaji wa chanjo ya Covid-19 duniani.

Rais Kagame amesema hayo katika ujumbe wa Twitter baada ya Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Tedros Adhanom Ghebreyesus, kusema kwamba mkataba ulioafikiwa kati ya mataifa tajiri na watengenezaji wa chanjo umefanya kuwa vigumu kwa shirika hilo kupata chanjo kwa ajili ya mpango wake wa Covax.

Covax ni mpango wa kuhakikisha kuna usambazaji sawa wa chanjo ya Covid-19 katika nchi zote duniani.

Mataifa tajiri yamekosolewa kwa kuhodhi chanjo na kufanya kuwa vigumu kwa nchi masikini kupata chanjo yoyote.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...