Jogoo aliyekuwa amefungwa kisu mguuni kwa ajili ya kupiganishwa na jogoo mwenzake amemuua mmiliki wake nchini India.
Tukio hilo limetokea katika jimbo la kusini mwa India la Telangana.
Kulingana na habari iliyotolewa na polisi, jogoo huyo, ambaye alikuwa amefungwa na kisu cha sentimita 8 kwenye miguu yake, alimjeruhi mmiliki wake kwenye kinena wakati akijaribu kuyakimbia mashindano.
Mwanaume huyo wa miaka 45 alipoteza maisha baada ya kupoteza damu nyingi..
Watu 15 walioshiriki katika vita vya jogoo wanatafutwa.

No comments:
Post a Comment