Kulingana na Ikulu ya Marekani, Biden na Mfalme Salman wamejadili kwa kirefu suala la usalama katika eneo la Ghuba na Mashariki ya Kati na pia wamekumbusha kuhusu umuhimu wa uhusiano kati ya Washington na Riyadh.
Mazungumzo kati ya viongozi hao yamefanyika wakati utawala wa Biden unatarajiwa kuchapisha leo ripoti ya siri iliyotayarishwa mwaka 2018 na mashirika ya ujasusi ya Marekani juu ya mauaji ya mwandishi habari wa Saudi Arabia, Jamal Khashoggi.
Ripoti hiyo ni sehemu ya uchunguzi mpana unaofichua kuwa mtoto wa mfalme Salman ambaye ni mrithi wa kiti cha ufalme Mohammed bin Salman aliidhinisha kuuwawa kwa Kashoggi nchini Uturuki, madai ambayo Saudi Arabia inakanusha.

No comments:
Post a Comment