Search This Blog

Sunday, February 7, 2021

Asimulia alivyopewa adhabu kwa saa mbili hadi ujauzito kuharibika

 


Asha Rajabu(28) mkazi wa kijiji cha Samanga Marangu wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, amesimulia namna alivyorukishwa kichurachura na mwenyekiti wa kijiji hicho, kwa madai ya kuchelewa kufunga baa na kusababisha ujauzito wake wa miezi miwili kuharibika.


Mwenyekiti huyo, Wilfredy Minja kwa sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo, kwa tuhuma ya kumsababishia Asha mateso na kupoteza ujauzito.


Akizungumza na gazeti hili, Asha alieleza kuwa kwa zaidi ya miaka mitano, amekuwa akisumbuka kutafuta ujauzito bila mafanikio mpaka hapo alipobahatika kuupata ujauzito huo, lakini baada ya kupata masaibu hayo, furaha yake imemtumbukia nyongo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...