Search This Blog

Wednesday, January 27, 2021

Wawakilishi wakutana kwenye awamu ya tano ya mazungumzo juu ya maandalizi ya katiba nchini Syria


Awamu ya tano ya mikutano ya Kamati ya Katiba ya Syria inaendelea katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa (UN) mjini Geneva.

Kikao cha siku ya tatu cha wanachama wa "kikundi kidogo" kinachohusika maandalizi ya katiba kinachojumuisha wanachama 15 kutoka kwa utawala wa Assad, mashirika ya umma na wawakilishi wa upinzani wa Syria, kinaongozwa na Geir O. Pedersen, ambaye ni Mwakilishi Maalum wa UN kwa Syria.

Wapinzani wa Syria wanaendelea na mazungumzo hayo juu ya "kanuni za msingi za katiba", ambayo ni ajenda kuu katika awamu ya tano ya mazungumzo.

Majadiliano hayo ya awamu ya tano yanayofanyika ndani bila waandishi wa habari yatamalizika siku ya Ijumaa, Januari 29.

Pedersen, ambaye atafanya mkutano na waandishi wa habari siku hiyo hiyo, anatarajiwa kutoa taarifa juu ya tarehe na ajenda ya awamu ijayo ya mazungumzo.

Katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika mnamo Januari 22, Pedersen alitoa wito kwa vyama hivyo kuanza kuandika katiba vyovyote iwezekanavyo.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...