Wataalam wa Shirika la Afya Duniani, WHO leo wameitembelea hospitali moja ya Wuhan na kuanza uchunguzi kuhusu chimbuko la virusi vya corona.
Wataalam hao watalichunguza pia soko moja la chakula linalodaiwa kuwa ndipo virusi hivyo vilipoanzia.
Uchunguzi huo wa WHO umecheleweshwa na kumekuwa na hofu kuhusiana na kupata ushahidi mwaka mmoja baada ya virusi hivyo kuibuka katika mji huo wa China
. Timu hiyo ilikutana na maafisa wa China na wakaondoka katika hoteli yao mjini Wuhan. Maeneo yote yatakayotembelewa na wataalam hao bado hayajajulikana.

No comments:
Post a Comment