Umoja wa Mataifa (UN) umetangaza kusitisha haki za kupiga kura za nchi 7 ambazo hazijalipa deni la ada ya ushirika.
Miongoni mwa nchi hizo, ni Iran ambayo ina deni kubwa zaidi la ada ya ushiriki la dola milioni 16 na elfu 200.
Nchi nyingine ambazo haki zao za kupiga kura pia zimesimamishwa ni Niger, Libya, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kongo, Sudan Kusini na Zimbabwe.
Nchi hizi zinatakiwa kulipa angalau kiasi maalum cha deni lao la ada ya ushiriki ili kupata haki zao za kupiga kura.
Hati ya Umoja wa Mataifa ina uwezo wa kusitishwa haki za kupiga kura kwa nchi ambazo hazijalipa ada zao za miaka 2.
Bajeti ya kila mwaka ya Umoja wa Mataifa ni dola bilioni 3 milioni 200. Muungano huu pia hutumia bajeti ya dola bilioni 6 na nusu kwa shughuli za kulinda amani kila mwaka.
Mwaka jana, haki za kupiga kura za nchi za Venezuela, Lebanon, Yemen, Gambia, Tonga, Jamhuri ya Afrika yaKati na Lesotho zilisimamishwa kwa sababu ya kukataa kulipa ada ya ushiriki.

No comments:
Post a Comment