Algeria inajiandaa kufungua tena ubalozi wake katika mji mkuu wa Tripoli nchini Libya, ambao ulikuwa umefungwa kwa miaka 7 kwa sababu za kiusalama.
Katika taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Algeria, ilielezwa kuwa Waziri Sabri Bukadum alitembelea jengo la ubalozi wakati wa ziara yake ya Tripoli, kwa matarajio ya kuanzisha tena shughuli za kidiplomasia.
Taarifa hiyo ilisema kwamba Ubalozi wa Tripoli, uliokuwa umefungwa tangu 2014, utafunguliwa tena katika siku zijazo.
Katika taarifa hiyo, ilielezwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje Bukadum alifanya mkutano wa mazungumzo na Waziri Mkuu wa Libya Fayiz al-Serraj, Rais wa Baraza Kuu la Kitaifa Halid al-Mishri, Spika wa Baraza la Wawakilishi Hammude Siyala, manaibu wa Libya na Waziri wa Mambo ya Nje Muhammed Tahir Siyala.
Wakati wa mkutano huo, Waziri wa Algeria alisisitiza kuwa nchi yake imekuwa katika mshikamano na watu wa Libya tangu mwanzo wa mgogoro na kwamba suluhisho la kisiasa linapaswa kupatikana kupitia mazungumzo kati ya pande husika za Libya.
Msemaji wa Waziri Mkuu wa Libya Galib al-Zaklai, hapo awali alisema kuwa Bukadum aliwahi kujadili mchakato wa mazungumzo ya kisiasa, kiusalama na kiuchumi na Fayiz al-Serraj pamoja na Khalid al-Misri kwa ajili ya kutatua mzozo.

No comments:
Post a Comment