Waandamanaji huko Yerevan mj mkuu wa Armenia wameendelea na maandamano wakitaka Waziri Mkuu Nikol Pashinyan ajiuzulu.
Maandamano ambayo yalianza baada ya Armenia kukubali kushindwa dhidi ya Azerbaijan katika mapigano Nagorno-Karabakh, yanaendelea hadi hii leo.
Waandamanaji walikuwa wakipiga kelele wakimtaka waziri huyo kujiuzulu huku mapigano yakizuka kati ya waandamanaji na polisi.
Wananchi huko Armenia walianza maandamano mnamo Novemba 10, baada ya Pashinyan kukubali kushindwa dhidi ya Azerbaijan.

No comments:
Post a Comment