Search This Blog

Monday, January 11, 2021

Simba yaweka rekodi ya kufika fainal nyingi katika Kombe la Mapinduzi


Hatua ya nusu Fainali ya Mashindano ya Kombe la Mapinduzi zitachezwa

leo Jumatatu katika Uwanja wa Amaan kati ya Azam FC vs Yanga Sc

Saa 10:15 jioni na Simba Sc vs Namungo FC saa 2:15 Usiku .

Hayo ni Mashindano ya 15 tangu yalipoanzishwa rasmi mwaka 2007 ambapo

 Simba Sc na Mtibwa Sugar zinaongoza kucheza fainali nyingi zikicheza

mara 6 kila timu.

Simba ambayo imecheza fainali 6, tatu ikitwaa Ubingwa na 3 ikipoteza

 (2008,2011,2015,2017,2019 na 2020).

Mtibwa Sugar nayo imecheza fainali nyingi (6) za Mashindano hayo ambapo

 wameshinda 2 na kupoteza 4 (2007, 2008, 2010, 2015, 2016 na 2020).

Azam ikishika nafasi ya tatu kucheza fainali nyingi za Mashindano hayo

ambapo imecheza fainali 5 na zote imetwaa Ubingwa (2012, 2013, 2017, 2018 na 2019.

Yanga wamecheza fainali 2 wakishinda 1 na kupoteza 1 (2007 na 2011)

sawa sawa na URA ya Uganda ikicheza fainali 2 wakishinda 1 na wakipoteza 1 (2016 na 2018).



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...