Watu 90,000 waliokimbia ghasia katika Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) wamepewa hifadhi katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Maafisa wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) walitangaza kuwa idadi ya watu waliokimbia ghasia katika Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) na kuingia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imeongezeka hadi 90,000.
Wakibainisha kuwa wahamiaji hao walivuka mto Ubangi na kuhamia maeneo ya Ubangi ya Kaskazini, Ubangi ya Kusini na Bas Uele kaskazini magharibi mwa DRC, maafisa wa UNHCR walifahamisha kuwa na hali ya hofu juu ya kuendelea kwa wimbi la kwanza la uhamiaji lilianza mapema mwezi huu.
Uhamiaji wa kukimbilia nchi jirani kama vile Cameroon, Chad na Kongo, ulianza kutokana na hali ya vurugu katika nchi ya CAR.
Baada ya Mahakama ya Katiba ya CAR kukataa kukubali ombi la kugombea kwa kiongozi aliyeondolewa madarakani Francois Bozize katika uchaguzi wa urais kwa kutokana na "jaribio la uhalifu na mauaji ya halaiki" na "kujumuishwa katika orodha ya vikwazo ya Umoja wa Mataifa", mapigano makali yalianza kati ya serikali na vikundi vya silaha mnamo tarehe 18 Desemba 2020.
Serikali na UN zilimtuhumu Bozize, ambaye alitajwa kuwa mhusika wa mizozo hiyo na kudaiwa kutaka "kundaa mapinduzi".
Nchi hiyo ambayo takriban asilimia 80 inadhibitiwa na vikundi vya silaha, makundi ya waasi yaliyoko chini ya chama cha muungano wa wazalendo (CPC) yalianzisha harakati za kuuteka mji mkuu wa Bangui mnamo mwezi Desemba.

No comments:
Post a Comment