Na katika michezo, Morocco ilipata ushindi wa 1 - 0 dhidi ya Togo jana wakati ikilenga kuwa nchi ya kwanza kutetea Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani - CHAN. Bao la Morocco lilipatikana kupitia penalti iliyopigwa mara mbili na Yahya Jabrane.
Morocco ndio wanaopigiwa upatu kufanya vyema katika mashindano hayo pamoja na wenyeji Cameroon na mabingwa mara mbili Cameroon Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Katika mechi nyingine ya Kundi C, Rwanda ililazimisha sar ya bila kufungana na Uganda. Hii leo, Tanzania itashuka dimbani kupambana na Zambia wakati Guinea ikiangushana na Namibia.

No comments:
Post a Comment