Search This Blog

Friday, January 15, 2021

Marekani yaiweka kampuni ya mafuta ya China katika orodha nyeusi


Marekani imeiweka Kampuni ya Kitaifa ya Mafuta ya Pwani ya China (CNOOC) katika orodha nyeusi kwa madai kwamba inatishia usalama wake wa kitaifa.

Idara ya Biashara ya Marekani ilitangaza kuwa imejumuisha kampuni ya Wachina Skyrizon kwenye orodha ya kampuni zinazohusiana na jeshi.

Katika taarifa iliyotolewa na Wizara hiyo, imeelezwa kuwa kampuni zote mbili zinatishia usalama wa kitaifa wa Marekani.

Imeelezwa kuwa CNOOC ilisaidia China kutisha majirani zake katika Bahari ya Kusini ya China na Skyrizon inauwezo wa kutengeneza bidhaa kama injini za ndege za jeshi.

Katika taarifa yake juu ya suala hilo, Waziri wa Biashara wa Marekani Wilbur Ross alisema kuwa vitendo vya uzembe na uchokozi wa China katika Bahari ya Kusini ya China na teknolojia ya silaha ni tishio kwa usalama wa Marekani na jamii ya kimataifa.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...