Search This Blog

Tuesday, January 19, 2021

Makamu Mwenyekiti LAAC afunguka kuanza kwa mafunzo ya kamati yake


Kamati ya LAAC imeteuliwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai, na leo hii wajumbe wa kamati hiyo wameanza kupewa mafunzo ya wiki moja ya kuwajengea uwezo ili waweze kusimamia matumizi ya rasilimali za umma zinazopelekwa kwenye Halmashauri zetu zote 185 Tanzania.

Akizungumza jijini Dodoma Makamu Mwenyekiti wa LAAC ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukene, Selemani Zedi amesema watayatumia mafunzo hayo kikamilifu katika kuwatumikia watanzania 

" Kwa mujibu wa majukumu yetu kikanuni, tutahakikisha rasilimali za umma zinazopelekwa halmashauri zinatumika kama zilivyokusudiwa, na matumizi yote yanafanyika kwa mujibu wa sheria ya fedha ya Serikali za Mitaa.

Kama ambavyo tuliapa kuilinda Katiba yetu na kuwaahidi wananchi wetu kuwatumikia kwa nguvu zetu ndivyo tutakavyozilinda rasilimali zetu kwa wivu mkubwa," Amesema Mbunge Zedi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...