Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed ameahidi kumaliza migogoro ya kikabila na vurugu katika mkoa wa Benishangul Gumuz magharibi mwa nchi.
Ahmed alisema kuwa tatizo la usalama litatatuliwa na wahalifu watafikishwa mahakamani wakati alipokutana na wakaazi wa jimbo linalokumbwa na mashambulizi yanayoendeshwa na watu wasiojulikana na kupelekea mizozo ya kikabila.
Akisisitiza kwa wananchi wa Ethiopia kwamba "njia pekee ni kulinda umoja wa nchi", Ahmed alisema kuwa operesheni ya usalama iliyozinduliwa katika eneo hilo itasimamiwa bila upendeleo.
Ahmed pia alisema kwamba hatua muhimu zitachukuliwa dhidi ya wasimamizi wa eneo ambao wanashindwa kudumisha amani na utulivu.
Mwenyekiti wa Jimbo Ashadli Hassen, Waziri wa Amani Muferihat Kamil na Amiri Jeshi Mkuu Berhanu Jula pia walihudhuria mkutano huo.
Mashambulizi yamekuwa yakilenga kabila la Amhara haswa katika mkoa ambapo Bwawa la Hedasi lilisababisha mzozo kati ya nchi zilizoko maeneo ya bonde la Mto Nile.
Serikali inasema kwamba waasi wa Tigray People's Liberation Front (TPLF) walihusika katika mapigano ya eneo hilo, ambapo maelfu ya watu walihama makazi yao.

No comments:
Post a Comment