Waziri wa Afya Fahrettin Koca amesema kuwa watu 1,100,000 wanatarajiwa kufanyiwa chanjo kila siku nchini.
Baada ya chanjo za kwanza kuwasilishwa nchini Uturuki kutoka China, ratiba na mpangilio wa namna ya usambazaji na utolewaji wa chanjo hiyo imebainishwa.
Chanjo hiyo ya China kwanza itafanyiwa uchunguzi. Mchakato huo wa uchunguzi utachukuwa wiki 2. Vituo 27,000 vya Afya ya Familia vitachukua jukumu kubwa katika chanjo. Hospitali za serikali na taasisi za afya za kibinafsi pia zitatumika.
Waziri wa Afya Fahrettin Koca alitoa ufafanuzi kuhusu namna ya utoaji wa chanjo kama ifuatavyo:
“Kuna vituo 27,000 vya Afya ya Familia katika nchi yetu. Chanjo zote zitatolewa hapa. Ikiwa kila kituo kitafanya chanjo 10 kwa siku, hiyo ingefanya jumla ya chanjo 270,000 kwa siku. Ikiwa zitatolewa chanjo 40; Inakuwa jumla ya chanjo 1,080,000. Pia hakuna haja ya kuanzisha vituo vipya. Hospitali zetu ni za kawaida sana. Tuna taasisi za afya za kibinafsi. Tutatumia hospitali hizi zote kwa lengo hili. Kikosi chetu cha afya, kinaweza kufanyiwa chanjo katika mazingira ya polyclinic hadi saa 23.00 na 24.00."
Akikumbushia kuwa chanjo ya SinoVac haikuonyesha athari mbaya katika utafiti uliofanywa kwa waliojitolea nchini Uturuki, Koca alisema kwamba shughuli ya utoaji chanjo itafanyika zaidi miezi ya Januari, Februari na Machi.

No comments:
Post a Comment